Ubaguzi
ubaguzi
Submitted by Mwananchi on Tue, 2007-01-23 11:09. UbaguziJina
andrew R.Chale
Maoni
NI SWALA LA WADAU WA MASWALA YA UKIMWI KUANDAA MATAMASHA MBALIMBALI YAHUSIYO UKIMWI.Mara nyingi wamekua wakijitokeza wakilatibu kufanikisha matamasha haya NAKUPELEA KUACHA WENGINE hususani watoto yatima wazazi wao walio kufa kwaAJALI,TB,nk bali si kwaukimwi.hapa nimeonelea kutoa maoni yangu kwa uchungu.utakuta wadau wanatangaza matamasha yawatoto yatima wazazi wao walikufa kwa UKIMWI KWAKWELI WENGINE WANAUMIA SANAA.naomba waache
Simu
0717049824
UBAGUZI
Submitted by Mwananchi on Tue, 2006-11-28 08:45. UbaguziJina
ELIA MWANGA
Maoni
Mimi nafikiri kwamba bado swala la ubaguzi limekithiri katika nchi yetu ya Tanzania.Ubaguzi unajithihirisha wazi katika ajira, elimu na katika nyanja nyingine za kijamii. Katika swala la ajira bado kigezo kikubwa cha kupata ajira imekuwa ni kujuana na wala si sifa mtu alizonazo.Na haya yamekuwa yanafanywa na viongozi wakubwa tu ambao wako madarakani. Katika swala la elimu bado watoto wa maskini tumekuwa tukibaguliwa hasa katika elimu ya juu.Swala la serikali kutoa mkopo kwa asilimia sitini ni kuwafukuza watoto wa maskini wasio na uwezo wakujilipia.Viongozi ambao wapo serikalini hawana wasiwasi kwani wao kwa kipato chao asiilimia sitini sio tatizo.
Simu
UBAGUZI KAZINI !!
Submitted by Mwananchi on Thu, 2006-11-09 12:02. UbaguziJina
CLIFF - ARS
Maoni
<p>INASIKITISHA KUONA SEHEMU ZA KAZI KUNA UBAGUZI WA KIJINSIA. BAADHI YA MAENEO YA KAZI MABOSI WANAUME WAMEKUWA WANAPENDELEA WAFANYAKAZI WA KIKE HATA WAKIFANYA KOSA BADO WATATETEWA ILA AKIFANYA MWANAUME KITAKACHOFUATA NI KUPEWA BARUA YA ONYO !! HALI HII SIO NZURI KABISA !! INAVUNJA MOYO WA KUFANYA KAZI</p>
Simu
Mimba kwa wanafunzi.
Submitted by Mwananchi on Sun, 2006-09-17 14:44. Elimu | UbaguziJina
Soko - Kitangiri
Maoni
Nasikitika sana kwamba mtoto wa kike anaepata ujauzito akiwa shuleni hufukuzwa shule hivyo anakatisha masomo na matarajio yake ya baadae kwake ndio inakua mwisho lakini tukumbuke kua huyu mtoto anaepata ujauzito hawi pekeake kwenye hio starehe wanakua watu wawili yani msichana na mvulana. inakuaje basi afukuzwe msichana pekee nahuyu mvulana aendelee kusoma nafikiri tufungue macho tuone kama watu hawa wameshiriki tendo hilo basi wote wafukuzwe maana bila mvulana msichana huyo asingepata huo ujauzito. Wakati umefika kuwaendeleza hawa wanafunzi kama hio haiwzekani basi wavulana waalimu wafanyakazi hata walinzi nao pia wafukuzwe kazi wanazozifanya kama mtoto huyu wa kike anae achisha masomo yake.Tukumbuke kua kupata ujauzito sio chanzo cha kukosa elimu basi waendelee mara baada ya kujifungua ni vizuri kumpa haki ya msingi ya elimu mtoto huyu wa kike ili wsiwe tegemezi kwa maisha yake hapo baadae. Naomba viongozi wetu tuliangalie suala hili kwa mara nyingine kwani bila kufanya hivyo kutakua hakuna viongozi wakike wa nyadhifa mbalimbali hapo baadae kwani wengi wao watakua hawana elimu ya kutosha. Hvi tunakubali kwamba wanawake waendelee kunyanyasika mpaka lini? Nasema tusikubali kunyanyasika tuna uhuru wa kusema 'NO" pale ambapo hatutaki kudharauliwa kunyanyasika nasi pia tupewe heshima hata sisi ni binadamu kama hao wanaume.
