Haki
NGO'S
Submitted by Mwananchi on Tue, 2007-01-16 15:11. HakiJina
CHILLAH.
Maoni
NGO'S kuongozwa na wakuu wa idara mbalimbali serikalini ni kitendo cha kurudisha nyuma maendeleo ya jamii kwani kinazuia haki kwa watu wa tabaka la chini wenye uwezo wa kuendesha miradi.
Simu
0755-162952
Janet, Tabora
HakiEeh kero kubwa ni upande wa sisi wajane unapoachwa na mume wako, unakuta familia ya mume wako ndio inakuja kukunyang'anya mali na kila kitu halafu inakuwacha na watoto yatima utunze mwenyewe. Wakati hao ndugu hawakuchangia chochote katika maendeleo yetu ya mimi na mume wangu.
My biggest concern is about us widows, when you loose your husband you find that the family of your husband comes and takes away the possessions and every thing else, leaving you to take care of the orphans by yourself. Even though they did not contribute in any way to the development of me and my husb
Latifa, Dar es Salaam
HakiMaoni yangu ni kwa Mashirika yanayohusika na haki za binaadam, kukemea suala la usafirishaji wa watoto hususan wa kike, kutoka Vijijini kuja Mijini kama wafanyakazi wa ndani kwani huu ni ukiukwaji wa haki za binaadam.
My opinion is directed towards the human rights organisations: to address the issue of child trafficking and especially the girls who are brought from the villages into towns to work as house girls, which is a violation of human rights.
Mafao ya NSSF
Submitted by Mwananchi on Wed, 2006-11-29 11:40. HakiJina
J.M.L, Arusha
Maoni
Kutokana na mfumuko wa bei ya kila kitu sisi wanachama wa NSSF tunaomba fursa ya kuchukua fedha kwenye akaunti zetu angalao mara moja kwa mwaka.Kwa utaratibu wa sasa fedha zetu zinapungua thamani kabla hatujazitumia.Ukiwekwa utaratibu mzuri tutaweza kusomesha watoto wetu ukizingatia elimu kwa mtoto haisubiri mzazi astaafu au kusimamishwa kazi vivyo hivyo ujenzi wa nyumba bora ni vizuri tujenge kabla ya kustaafu.Mfano umechangia NSSF kwa mika kumi,thamani ya miaka nane itakua imeanguka sana.Hivyo ni FAIDA ZAIDI kutumia hizo fedha KILA MWAKA.KWA MPANGO HUO TUTAONA FAIDA YA NSSF.
Simu
haki zizigatiwe kwa Asasi zote zinazo shughulika na ukimwi nchini tanzania
Submitted by Mwananchi on Tue, 2006-09-05 14:41. Afya | HakiJina
Ayubu samweli
Maoni
Nikwamba mimi nasikia uchungu sana ninapo ona serikali za almashauli zinapo toa fedha kwa asasi zisizo Sajiliwa, Na asasi zilizo sajiliwa hazipewi kwasababu kanunu ya tanzania inasema mtu yoyote anaye azisha kitu kama asassi lazima asajiliwe. pasipo kusajiliwa huyo nitapeli .nawatanzania wengisana wametapeliwa asante ni MIMI .AYUBU SAMWELI . TOKA MTWRA COCOBEACH
Simu
255, 23,2333355,
Sulemida, Lushoto
Ajira | HakiNingependa kuwa mwanasheria... nimependa kazi hii kwa sababu ni wachache ambao wanatendewa haki. Ukichukulia wasichana, mtu anaenda kuomba kazi sehemu anaambiwa kama sio jinsi yake, aliyemkuta anamwambia "nifanyie mapenzi ili nikupe kazii" Hawa, mimi ningekuwa mwanasheria, ningeona ni haki ya msichana apewe kazi endapo ana elimu inayohusiana na kazi hiyo.
I'd like to be a lawyer... I like this profession because here, few people are treated with justice. Take girls for example, a girl asks for a job some place but is told that it's not the way it is, the employer tells her "make love with me first if you want the job". If I was a lawyer, I would see to that this girl has a right to that job as long as she is qualified for it.
